News
Rais Mwinyi aizawadia Yanga Milioni 100

News
Stan Bakora achukuwa fomu kugombea udiwani Morogoro Mjini

Na Mwandishi wetu, News Info Online
Msanii Stanbakora amechukua Fomu ya kuomba ridhaa ya Kugombea Udiwani Morogoro Mjini Kata ya Kiwanja Cha Ndege kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kupitia ukurasa wake Instagram ameandika.
“Wana MOROGORO MJINI Kata Ya KIWANJA CHA NDEGE Nipo Tayar Kuwatumikia”

SatMediaUpdates
News
Zahoro Hanuna Achukua Fomu ya Kugombea Ubunge Bumbuli Kupitia CCM

Na Mwandishi wetu, News Info Online
Zahoro Rashid Hanuna, leo Juni 28, 2025, amechukua rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hanuna alipowasili katika Ofisi za CCM Wilaya ya Lushoto, mkoani Tanga, alipokelewa na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mhe. M.S. Kaaya, ambaye alimkabidhi rasmi fomu ya kugombea nafasi hiyo.
Hanuna si mgeni katika siasa za ndani ya CCM. Mwaka 2020 aligombea kura za maoni katika Jimbo la Kawe, na mwaka 2021 alijitokeza kuwania nafasi ya uspika wa Bunge kupitia chama hicho.
Hatua yake ya kuchukua fomu leo inaashiria mwendelezo wa safari yake ya kisiasa, akilenga kuwawakilisha wananchi wa Bumbuli bungeni kupitia tiketi ya CCM



News
FCC YATOA SEMINA YA MASUALA YA UHIBITI BANDIA KWA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online
Tume ya Ushindani (FCC) imeendesha semina maalum ya Uhamasishaji wa masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa Bidhaa bandia kwa wanawake wajasiriamali Mkoa wa Dar es Salaam, kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo Sheria zinazosimamia masuala ya Ushindani nchini.
Semina hiyo ya siku moja imefanyika June 13, 2025 katika Ofisi za FCC Jijini Dar es Salaa, kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) kuelewa zaidi sheria na kanuni za ushindani wa haki zitakazosaidia kufanya shughuli zao kwa weledi.
Akizungumza alipokuwa akifungua kikao hicho, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa, Mkurugenzi wa Tafiti, Muungano wa Makampuni na Uraghibishi Bi. Zaytun Kikula, amesema mafunzo hayo yana mchango mkubwa katika kuimarisha mazingira ya Biashara nchini.
“Jukwaa hili linaturuhusu kushirikiana moja kwa moja na wamiliki wa biashara, kuwaelimisha juu ya sheria za ushindani, na kuhakikisha wanajenga biashara imara na endelevu,” alisema.

Aidha, Bi. Kikula amesema anaamini kuwa wafanyabiashara wanawake wana nafasi kubwa katika maendeleo ya kiuchumi, ustawi wa familia na ukuaji wa jamii, nakwamba utowawezesha kuna athari ya moja kwa moja kwa jamii.
Amesisitiza kuwa kulinda biashara dhidi ya ushindani usio wa haki, pamoja na kuhakikisha wateja wanapokea bidhaa na huduma bora, inasalia kuwa sehemu ya msingi ya mamlaka ya FCC.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa TWCC Bi. Mwalongo Kambewe amewataka washiriki kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha shuguli zao, huku akibainisha kuwa maarifa huleta mabadiliko
Kila unapojifunza unakua” Bi. Kambewe amesema na kuongeza kuwa “Ninaamini wanawake hawa wataona mabadiliko sio tu katika biashara zao bali hata katika familia na jamii zao. amesema.
Naye Kaimu Meneja wa Makubaliano ya Washindani wa FCC, Bw. David Mawi, akizungumza alipokuwa akitoa wasilisho katika semina hiyo, amesisitiza kuwa soko huria haliwezi kuendelea bila kuwepo udhibiti.
“Soko huria haliwezi kuendelea bila mdhibiti, Tunahitaji kulinda biashara na watumiaji dhidi ya mazoea yasiyo ya haki ambayo mara nyingi yanalenga washiriki wadogo au wapya kwenye soko.” Amesema Bw. Mawi

Ameongeza kuwa kutumia vibaya utawala wa soko, unaofafanuliwa kama kudhibiti zaidi ya asilimia 40 ya hisa ya soko kwa muda endelevu, ni ukiukaji wa sheria na hatari ya kuwadhuru washindani na watumiaji.
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za FCC katika kuhakikisha wajasiriamali wanawake wa Kitanzania wanapata maarifa na kujengewa uelewa ili kufanikiwa katika soko la ushindani, ndani na nje ya nchi.
-
News11 months ago
Major Sporting Events and International Competitions
-
Uncategorized2 months ago
NMB Foundation yawanoa Wakulima wa Zao la Kakao Kyela, Serikali yaipongeza
-
News1 month ago
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini
-
Uncategorized2 months ago
NMB Yaandika Historia kwa Kushinda Tuzo Sita Kubwa, Ikiwemo ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika”
-
Politics11 months ago
Elections 2024: Key Issues and Candidates to Watch
-
News3 weeks ago
FCC YATOA SEMINA YA MASUALA YA UHIBITI BANDIA KWA WAJASIRIAMALI WANAWAKE
-
Health11 months ago
Physical Activity for Everyone: Exercise Tips for Different Ages and Abilities
-
Health11 months ago
Mental Health Awareness: Why It Matters More Than Ever