Connect with us

News

Makonda tunakwenda kuchechemua uchumi wa Arusha kwa kuwekeza kwenye miundombinu na Ajira

Published

on

Na Mwandishi wetu, NewsInfo – Arusha

Mgombea ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amesema dhamira yake ni kuhakikisha Arusha inakuwa kitovu cha uchumi kwa kuwekeza kwenye maeneo ya viwanda, miundombinu, huduma bora kwa wananchi na ujenzi wa mazingira rafiki ya kiuchumi.

Akizungumza na wananchi wa Arusha, Makonda alisema kuwa eneo la viwanda ndilo linalotoa fursa kubwa ya ajira na kuinua kipato cha wananchi, hivyo Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kulipa kipaumbele kwa kujenga viwanja vya AFCON, kumbi za mikutano na maeneo ya uwekezaji ambayo yote yanalenga kuleta wageni, kuongeza mzunguko wa fedha na kuchochea ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Arusha.

Makonda aliongeza kuwa eneo la pili lenye umuhimu mkubwa ni miundombinu, ikiwemo maji, shule, afya, barabara na kumbi mbalimbali. Alisema ujenzi wa miundombinu imara ni nguzo ya maendeleo na ndio msingi wa uchumi endelevu.

“Juzi nilikwenda kuangalia Bandari ya Dar es Salaam, Rais Samia amewekeza kwa kiwango kikubwa. Tumeona mizigo ikiongezeka kutoka tani milioni 18 hadi milioni 27 kwa mwaka. Siyo tu bandari ya Dar es Salaam, bali pia Mtwara imeongezeka kutoka tani 590,000 hadi milioni 2.59, na Tanga kutoka tani 830,000 hadi milioni 1.3. Hii inaonesha namna uwekezaji unavyokuza uchumi,” alisema Makonda.

Ameeleza kuwa katika miaka mitano ijayo, ataweka mkazo katika kuboresha huduma kwa wananchi kwa kuzingatia kaulimbiu ya mgombea urais wa CCM, “Kazi na Utu.”

“Kazi ni ile inayojenga uchumi na kuboresha mazingira, lakini utu ni kumthamini kila mtu kwa heshima bila kujali kipato chake,” alisema Makonda.

Aidha, Makonda aliahidi kuwa Jimbo la Arusha Mjini litakuwa namba moja kwa watu kupata haki zao, akisema hataki kuona wanawake wakinyanyasika wanapofika hospitalini au wananchi wanapokwenda kwenye serikali za mitaa na vituo vya polisi.

“Hatutambagua mtu. Tutahakikisha kila mmoja anaheshimika, anapata haki yake na kutimiza wajibu wake. Hiyo ndiyo ndoto yetu,” alisisitiza.

Makonda alisema awamu inayofuata ya miaka mitano itakuwa ni ya kuuchechemua uchumi wa Arusha, kuhakikisha kila eneo lenye fursa ya kiuchumi linatumiwa vizuri ili wananchi wa Arusha wawe na kipato cha uhakika.

Akiwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi tarehe 29 kupiga kura, Makonda alisema ni muhimu kumchagua kiongozi mwenye uwezo, busara na uzoefu wa kulinda uchumi, diplomasia na usalama wa nchi kama alivyoonyesha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Tulipopoteza Rais, taifa halikugawanyika kwa sababu tulikuwa na mwanamama mwenye maono makubwa na utulivu wa hali ya juu. Tumepita salama kwa uimara wake,” alisema.

Akizungumzia maandamano yanayotangazwa na baadhi ya watu mitandaoni, Makonda alisema taarifa alizonazo zinaonyesha kwamba waliohusika walikuwa wakitafuta fedha, na sasa wamekwisha kukosa ufadhili.

“Niliwaambia watu Kariakoo, mtu akikushawishi uache kazi yako ukaandamane, mwambie aniambie kwanza nipe pesa yangu kabla sijaacha kazi ninayoniingizia kipato,” alisema Makonda.

Alimalizia kwa kusema kuwa wananchi wa Arusha wanapaswa kuchagua maendeleo, umoja na ustawi wa watu kupitia kazi na utu, si maneno ya mitandaoni.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.