News
Dkt. Biteko akutana na Mtendaji Mkuu wa PUMA Duniani

News
FCC YATOA SEMINA YA MASUALA YA UHIBITI BANDIA KWA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online
Tume ya Ushindani (FCC) imeendesha semina maalum ya Uhamasishaji wa masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa Bidhaa bandia kwa wanawake wajasiriamali Mkoa wa Dar es Salaam, kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo Sheria zinazosimamia masuala ya Ushindani nchini.
Semina hiyo ya siku moja imefanyika June 13, 2025 katika Ofisi za FCC Jijini Dar es Salaa, kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) kuelewa zaidi sheria na kanuni za ushindani wa haki zitakazosaidia kufanya shughuli zao kwa weledi.
Akizungumza alipokuwa akifungua kikao hicho, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa, Mkurugenzi wa Tafiti, Muungano wa Makampuni na Uraghibishi Bi. Zaytun Kikula, amesema mafunzo hayo yana mchango mkubwa katika kuimarisha mazingira ya Biashara nchini.
“Jukwaa hili linaturuhusu kushirikiana moja kwa moja na wamiliki wa biashara, kuwaelimisha juu ya sheria za ushindani, na kuhakikisha wanajenga biashara imara na endelevu,” alisema.

Aidha, Bi. Kikula amesema anaamini kuwa wafanyabiashara wanawake wana nafasi kubwa katika maendeleo ya kiuchumi, ustawi wa familia na ukuaji wa jamii, nakwamba utowawezesha kuna athari ya moja kwa moja kwa jamii.
Amesisitiza kuwa kulinda biashara dhidi ya ushindani usio wa haki, pamoja na kuhakikisha wateja wanapokea bidhaa na huduma bora, inasalia kuwa sehemu ya msingi ya mamlaka ya FCC.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa TWCC Bi. Mwalongo Kambewe amewataka washiriki kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha shuguli zao, huku akibainisha kuwa maarifa huleta mabadiliko
Kila unapojifunza unakua” Bi. Kambewe amesema na kuongeza kuwa “Ninaamini wanawake hawa wataona mabadiliko sio tu katika biashara zao bali hata katika familia na jamii zao. amesema.
Naye Kaimu Meneja wa Makubaliano ya Washindani wa FCC, Bw. David Mawi, akizungumza alipokuwa akitoa wasilisho katika semina hiyo, amesisitiza kuwa soko huria haliwezi kuendelea bila kuwepo udhibiti.
“Soko huria haliwezi kuendelea bila mdhibiti, Tunahitaji kulinda biashara na watumiaji dhidi ya mazoea yasiyo ya haki ambayo mara nyingi yanalenga washiriki wadogo au wapya kwenye soko.” Amesema Bw. Mawi

Ameongeza kuwa kutumia vibaya utawala wa soko, unaofafanuliwa kama kudhibiti zaidi ya asilimia 40 ya hisa ya soko kwa muda endelevu, ni ukiukaji wa sheria na hatari ya kuwadhuru washindani na watumiaji.
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za FCC katika kuhakikisha wajasiriamali wanawake wa Kitanzania wanapata maarifa na kujengewa uelewa ili kufanikiwa katika soko la ushindani, ndani na nje ya nchi.
News
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini

Na Mwandishi wetu, NewsInfo Online
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ametangaza kuwa Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan itatumia kiasi cha Shilingi Bilioni 669 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja katika mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kuboresha usafiri na kuifungua mikoa hiyo kiuchumi.
Akizungumza mkoani Mtwara, Ulega alisema barabara na madaraja hayo yatajengwa kupitia barabara za Mtwara –Mingoyo (Mnazi mmoja)-Masasi (km 201) itakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 401 huku barabara nyingine ya Mtwara Tandahimba-Newala-Masasi itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 268 hadi kukamilika kwake.
Waziri Ulega amewaambia wananchi wa Mtwara kwamba kiasi hicho kikubwa cha fedha katika ujenzi wa miundombinu hiyo unaonyesha dhamira ya dhati aliyonayo Rais Samia kwa wananchi wa Mikoa ya Kusini na lengo kubwa ni kuhakikisha inafunguka kiuchumi na kuwapa wananchi fursa za kiuchumi.
“Wananchi wa mikoa ya Kusini, ninawaletea salamu hizi za Rais wenu Samia Suluhu Hassan. Hizi barabara zikikamilika kutakuwa na taa za barabarani takribani 4800 kutoka Mtwara hadi Masasi. Kusini kutang’ara kwa mwanga nyakati za usiku na kutapendeza. Kwenye barabara nzuri, uchumi unafunguka na kwenye mwanga kwa saa 24, biashara zinafanyika muda wote,”alisema Ulega.
Ulega yuko katika ziara ya kikazi mkoani Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine anafuatilia maagizo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kuangalia maendeleo ya ukarabati wa barabara na miundombinu mingine ya ujenzi iliyoharibiwa wakati wa mvua za masika na kimbunga cha Hidaya kuanzia mwishoni mwa mwaka jana hadi mwaka huu.
Akitoa mchanganuo, Ulega alisema katika kiasi hicho cha fedha, zaidi ya shilingi bilioni 230 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Mnivata – Newala – Masasi (km 160) kwa kiwango cha lami pamoja na Daraja la Mwiti (m 84) ili kuzifungua Wilaya za Masasi, Newala, Tandahimba na Mtwara kiuchumi kupitia usafirishaji wa abiria na mazao.
Ulega amewataka Makandarasi wanaojenga barabara ya Mnivata-Masasi kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi wazawa wa maeneo barabara inakopita kwa kushirikisha ofisi za Serikali za Mtaa na Kata za Wilaya.
Amesisitiza kuwa licha ya Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya barabara, miradi hiyo inapaswa kuzalisha ajira kwa wananchi wazawa na kuacha ujuzi ili uweze kuwasaidia katika majukumu mengine ya kijamii na kiuchumi.
Ulega ameitaka TANROADS kukamilisha taratibu za kuwapata wakandarasi watakaotekeleza miradi Jumuishi ya kijamii (CSR) ili ujenzi wa barabara uende sambamba na miradi hiyo ambayo itahusisha ujenzi wa Kituo cha Mabasi, ghala, ununuzi wa mashine za kubangulia korosho, mabweni ya shule, nyumba za madaktari, ununuzi wa X-Ray na gari la wagonjwa.
Naye, Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Dotto John ameeleza mradi huo unaotekelezwa na Mkandarasi China WuYi umegawanywa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza ya Mnivata – Mitesa (km 100) unatekelezwa kwa muda wa miezi 36 na sehemu ya pili ya Mitesa – Masasi (km 60) na ujenzi wa Daraja la Mwiti (m 84) unatekelezwa kwa muda wa miezi 30.
Kwa upande wake, Mbunge wa Tandahimba Ahmad Katani ameishukuru Serikali kwa mradi wa barabara hiyo kwani ni barabara ya kiuchumi kwa kuwa inapita katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa Korosho.


News
NMB Yatua Mafinga na Kasulu kwa Kijiji Day, Yaendelea Kusambaza Elimu ya Fedha

Na Mwandishi Wetu, NewsInfo Online
Benki ya NMB imeendelea na programu yake ya NMB Kijiji Day kwa kishindo, ambapo matukio mawili makubwa yamefanyika kwa siku moja katika vijiji vya Igowole, Mafinga mkoani Iringa na Rusesa, Kasulu mkoani Kigoma, yakiambatana na utoaji wa elimu ya fedha, huduma za kifedha, elimu ya nishati safi ya kupikia, na kampeni za mazingira.
Katika kijiji cha Igowole, Mafinga, wakazi walipata fursa ya kushiriki katika warsha za elimu ya fedha kupitia mkakati maalum wa Nondo za Pesa, unaolenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma rasmi za kifedha. Elimu hiyo ilijumuisha huduma za kufungua akaunti, mikopo, bima na matumizi ya huduma za kidijitali.
Mbali na elimu ya kifedha, tukio hilo lilihusisha semina juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia, mafunzo kwa vyama vya kijamii, burudani kupitia bonanza lenye michezo mbalimbali, na upandaji wa miti zaidi ya 600 kwa ajili ya kuhifadhi mazingira.
Benki iliwakilishwa na Manyilizu Masanja, Meneja wa Mauzo wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, kwa niaba ya Meneja wa Kanda.
Wakati huo huo, katika kijiji cha Rusesa, Kasulu, NMB Kijiji Day ilipamba moto kwa kuwahusisha zaidi ya vikundi 20 vya kijamii vyenye wanachama zaidi ya 600, waliopatiwa elimu juu ya huduma jumuishi za kifedha, nishati safi na utunzaji wa mazingira.
Katika tukio hilo, NMB ilikabidhi na kupanda miche 1,000 ya miti kwenye shule za msingi na sekondari za kijiji hicho, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake kwa Serikali ya Awamu ya Sita kupitia kampeni ya Milioni Moja Miti na mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Katibu Tarafa wa Buyonga Paul Ramadhan alisifu juhudi za NMB katika kuunga mkono mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kuhimiza matumizi ya nishati safi.
“NMB wametushika mkono leo. Tumeshuhudia elimu, michezo, na kampeni za mazingira, all in one. Huu ni mfano bora wa taasisi binafsi kushiriki maendeleo ya jamii,” alisema Ramadhan.
Kwa upande wake, Meneja wa Tawi la NMB Kasulu, Ipyana Mwakatobe, alieleza kufurahishwa na mwamko wa wananchi na kuahidi kuendelea kushirikiana nao ili kukuza ustawi wa kiuchumi, kiafya na kielimu katika wilaya hiyo.
Katika bonanza lililoambatana na sherehe hizo, wakazi wa Rusesa walishiriki michezo mbalimbali ikiwemo kuvuta kamba, mpira wa miguu, mbio za baiskeli, na michezo ya jadi kama bao na drafti. Mechi ya fainali ya mpira wa miguu iliwashuhudia wenyeji Rusesa City FC wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya New Generation Academy ya Kasulu.
NMB inatarajia kufikia zaidi ya vijiji 2,000 kupitia Kijiji Day mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia Watanzania wote, hata walioko vijijini.






-
News10 months ago
Major Sporting Events and International Competitions
-
Science12 months ago
Space Exploration: Recent Discoveries and Future Missions
-
Uncategorized4 weeks ago
NMB Foundation yawanoa Wakulima wa Zao la Kakao Kyela, Serikali yaipongeza
-
Politics11 months ago
Elections 2024: Key Issues and Candidates to Watch
-
Uncategorized1 month ago
NMB Yaandika Historia kwa Kushinda Tuzo Sita Kubwa, Ikiwemo ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika”
-
News3 weeks ago
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini
-
Health10 months ago
Mental Health Awareness: Why It Matters More Than Ever
-
Science11 months ago
Interview with a Scientist: Exploring Cutting-Edge Research