News
New International Agreements Strengthen Global Cooperation
Several countries have recently signed new international agreements designed to enhance global cooperation in areas such as trade, security, and environmental protection. These agreements aim to foster stronger diplomatic ties, boost economic growth, and address global challenges through collaborative efforts.

News
FCC YATOA SEMINA YA MASUALA YA UHIBITI BANDIA KWA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online
Tume ya Ushindani (FCC) imeendesha semina maalum ya Uhamasishaji wa masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa Bidhaa bandia kwa wanawake wajasiriamali Mkoa wa Dar es Salaam, kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo Sheria zinazosimamia masuala ya Ushindani nchini.
Semina hiyo ya siku moja imefanyika June 13, 2025 katika Ofisi za FCC Jijini Dar es Salaa, kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) kuelewa zaidi sheria na kanuni za ushindani wa haki zitakazosaidia kufanya shughuli zao kwa weledi.
Akizungumza alipokuwa akifungua kikao hicho, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa, Mkurugenzi wa Tafiti, Muungano wa Makampuni na Uraghibishi Bi. Zaytun Kikula, amesema mafunzo hayo yana mchango mkubwa katika kuimarisha mazingira ya Biashara nchini.
“Jukwaa hili linaturuhusu kushirikiana moja kwa moja na wamiliki wa biashara, kuwaelimisha juu ya sheria za ushindani, na kuhakikisha wanajenga biashara imara na endelevu,” alisema.

Aidha, Bi. Kikula amesema anaamini kuwa wafanyabiashara wanawake wana nafasi kubwa katika maendeleo ya kiuchumi, ustawi wa familia na ukuaji wa jamii, nakwamba utowawezesha kuna athari ya moja kwa moja kwa jamii.
Amesisitiza kuwa kulinda biashara dhidi ya ushindani usio wa haki, pamoja na kuhakikisha wateja wanapokea bidhaa na huduma bora, inasalia kuwa sehemu ya msingi ya mamlaka ya FCC.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa TWCC Bi. Mwalongo Kambewe amewataka washiriki kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha shuguli zao, huku akibainisha kuwa maarifa huleta mabadiliko
Kila unapojifunza unakua” Bi. Kambewe amesema na kuongeza kuwa “Ninaamini wanawake hawa wataona mabadiliko sio tu katika biashara zao bali hata katika familia na jamii zao. amesema.
Naye Kaimu Meneja wa Makubaliano ya Washindani wa FCC, Bw. David Mawi, akizungumza alipokuwa akitoa wasilisho katika semina hiyo, amesisitiza kuwa soko huria haliwezi kuendelea bila kuwepo udhibiti.
“Soko huria haliwezi kuendelea bila mdhibiti, Tunahitaji kulinda biashara na watumiaji dhidi ya mazoea yasiyo ya haki ambayo mara nyingi yanalenga washiriki wadogo au wapya kwenye soko.” Amesema Bw. Mawi

Ameongeza kuwa kutumia vibaya utawala wa soko, unaofafanuliwa kama kudhibiti zaidi ya asilimia 40 ya hisa ya soko kwa muda endelevu, ni ukiukaji wa sheria na hatari ya kuwadhuru washindani na watumiaji.
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za FCC katika kuhakikisha wajasiriamali wanawake wa Kitanzania wanapata maarifa na kujengewa uelewa ili kufanikiwa katika soko la ushindani, ndani na nje ya nchi.
News
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini

Na Mwandishi wetu, NewsInfo Online
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ametangaza kuwa Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan itatumia kiasi cha Shilingi Bilioni 669 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja katika mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kuboresha usafiri na kuifungua mikoa hiyo kiuchumi.
Akizungumza mkoani Mtwara, Ulega alisema barabara na madaraja hayo yatajengwa kupitia barabara za Mtwara –Mingoyo (Mnazi mmoja)-Masasi (km 201) itakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 401 huku barabara nyingine ya Mtwara Tandahimba-Newala-Masasi itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 268 hadi kukamilika kwake.
Waziri Ulega amewaambia wananchi wa Mtwara kwamba kiasi hicho kikubwa cha fedha katika ujenzi wa miundombinu hiyo unaonyesha dhamira ya dhati aliyonayo Rais Samia kwa wananchi wa Mikoa ya Kusini na lengo kubwa ni kuhakikisha inafunguka kiuchumi na kuwapa wananchi fursa za kiuchumi.
“Wananchi wa mikoa ya Kusini, ninawaletea salamu hizi za Rais wenu Samia Suluhu Hassan. Hizi barabara zikikamilika kutakuwa na taa za barabarani takribani 4800 kutoka Mtwara hadi Masasi. Kusini kutang’ara kwa mwanga nyakati za usiku na kutapendeza. Kwenye barabara nzuri, uchumi unafunguka na kwenye mwanga kwa saa 24, biashara zinafanyika muda wote,”alisema Ulega.
Ulega yuko katika ziara ya kikazi mkoani Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine anafuatilia maagizo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kuangalia maendeleo ya ukarabati wa barabara na miundombinu mingine ya ujenzi iliyoharibiwa wakati wa mvua za masika na kimbunga cha Hidaya kuanzia mwishoni mwa mwaka jana hadi mwaka huu.
Akitoa mchanganuo, Ulega alisema katika kiasi hicho cha fedha, zaidi ya shilingi bilioni 230 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Mnivata – Newala – Masasi (km 160) kwa kiwango cha lami pamoja na Daraja la Mwiti (m 84) ili kuzifungua Wilaya za Masasi, Newala, Tandahimba na Mtwara kiuchumi kupitia usafirishaji wa abiria na mazao.
Ulega amewataka Makandarasi wanaojenga barabara ya Mnivata-Masasi kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi wazawa wa maeneo barabara inakopita kwa kushirikisha ofisi za Serikali za Mtaa na Kata za Wilaya.
Amesisitiza kuwa licha ya Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya barabara, miradi hiyo inapaswa kuzalisha ajira kwa wananchi wazawa na kuacha ujuzi ili uweze kuwasaidia katika majukumu mengine ya kijamii na kiuchumi.
Ulega ameitaka TANROADS kukamilisha taratibu za kuwapata wakandarasi watakaotekeleza miradi Jumuishi ya kijamii (CSR) ili ujenzi wa barabara uende sambamba na miradi hiyo ambayo itahusisha ujenzi wa Kituo cha Mabasi, ghala, ununuzi wa mashine za kubangulia korosho, mabweni ya shule, nyumba za madaktari, ununuzi wa X-Ray na gari la wagonjwa.
Naye, Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Dotto John ameeleza mradi huo unaotekelezwa na Mkandarasi China WuYi umegawanywa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza ya Mnivata – Mitesa (km 100) unatekelezwa kwa muda wa miezi 36 na sehemu ya pili ya Mitesa – Masasi (km 60) na ujenzi wa Daraja la Mwiti (m 84) unatekelezwa kwa muda wa miezi 30.
Kwa upande wake, Mbunge wa Tandahimba Ahmad Katani ameishukuru Serikali kwa mradi wa barabara hiyo kwani ni barabara ya kiuchumi kwa kuwa inapita katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa Korosho.


News
Dkt. Biteko akutana na Mtendaji Mkuu wa PUMA Duniani

Na Mwandishi wetu, NewsInfo Online
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Duniani Bw. Mark Russell.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Mei 27, 2025 jijini Dodoma, Dkt. Biteko ameipongeza Kampuni ya PUMA Energies kwa kuwekeza nchini na kutoa huduma ya viwango vya juu katika bidhaa zake pamoja na kuzingatia wazawa katika nafasi za juu za utendaji za Kampuni hiyo nchini.
Vilevile, ametoa rai kwa PUMA Energies kuendelea kuwekeza zaidi nchini na kusema kuwa Kampuni hiyo inaweza kujenga vituo zaidi vya kuweka gesi kwenye magari ili kusaidia upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Kuhusu nishati safi ya kupikia, Dkt. Biteko ametoa wito kwa Kampuni ya PUMA kuwekeza katika eneo hilo na kusema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano wake kwa Kampuni hiyo.
Naye, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Bw. Mark Russell amesema kuwa Kampuni yake imewekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 24 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vitatu vya kujaza gesi kwenye magari katika mikoa ya Dar es salaam na kimoja Dodoma.


-
News10 months ago
Major Sporting Events and International Competitions
-
Science12 months ago
Space Exploration: Recent Discoveries and Future Missions
-
Uncategorized4 weeks ago
NMB Foundation yawanoa Wakulima wa Zao la Kakao Kyela, Serikali yaipongeza
-
Politics11 months ago
Elections 2024: Key Issues and Candidates to Watch
-
Uncategorized1 month ago
NMB Yaandika Historia kwa Kushinda Tuzo Sita Kubwa, Ikiwemo ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika”
-
News3 weeks ago
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini
-
Health10 months ago
Mental Health Awareness: Why It Matters More Than Ever
-
News3 weeks ago
Dkt. Biteko akutana na Mtendaji Mkuu wa PUMA Duniani