News
Rais Samia apeleka Bilioni 669 za Barabara, Madaraja mikoa ya Kusini

News
FCC YATOA SEMINA YA MASUALA YA UHIBITI BANDIA KWA WAJASIRIAMALI WANAWAKE

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online
Tume ya Ushindani (FCC) imeendesha semina maalum ya Uhamasishaji wa masuala ya ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa Bidhaa bandia kwa wanawake wajasiriamali Mkoa wa Dar es Salaam, kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo Sheria zinazosimamia masuala ya Ushindani nchini.
Semina hiyo ya siku moja imefanyika June 13, 2025 katika Ofisi za FCC Jijini Dar es Salaa, kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), ili kuwawezesha wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs) kuelewa zaidi sheria na kanuni za ushindani wa haki zitakazosaidia kufanya shughuli zao kwa weledi.
Akizungumza alipokuwa akifungua kikao hicho, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa, Mkurugenzi wa Tafiti, Muungano wa Makampuni na Uraghibishi Bi. Zaytun Kikula, amesema mafunzo hayo yana mchango mkubwa katika kuimarisha mazingira ya Biashara nchini.
“Jukwaa hili linaturuhusu kushirikiana moja kwa moja na wamiliki wa biashara, kuwaelimisha juu ya sheria za ushindani, na kuhakikisha wanajenga biashara imara na endelevu,” alisema.

Aidha, Bi. Kikula amesema anaamini kuwa wafanyabiashara wanawake wana nafasi kubwa katika maendeleo ya kiuchumi, ustawi wa familia na ukuaji wa jamii, nakwamba utowawezesha kuna athari ya moja kwa moja kwa jamii.
Amesisitiza kuwa kulinda biashara dhidi ya ushindani usio wa haki, pamoja na kuhakikisha wateja wanapokea bidhaa na huduma bora, inasalia kuwa sehemu ya msingi ya mamlaka ya FCC.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa TWCC Bi. Mwalongo Kambewe amewataka washiriki kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha shuguli zao, huku akibainisha kuwa maarifa huleta mabadiliko
Kila unapojifunza unakua” Bi. Kambewe amesema na kuongeza kuwa “Ninaamini wanawake hawa wataona mabadiliko sio tu katika biashara zao bali hata katika familia na jamii zao. amesema.
Naye Kaimu Meneja wa Makubaliano ya Washindani wa FCC, Bw. David Mawi, akizungumza alipokuwa akitoa wasilisho katika semina hiyo, amesisitiza kuwa soko huria haliwezi kuendelea bila kuwepo udhibiti.
“Soko huria haliwezi kuendelea bila mdhibiti, Tunahitaji kulinda biashara na watumiaji dhidi ya mazoea yasiyo ya haki ambayo mara nyingi yanalenga washiriki wadogo au wapya kwenye soko.” Amesema Bw. Mawi

Ameongeza kuwa kutumia vibaya utawala wa soko, unaofafanuliwa kama kudhibiti zaidi ya asilimia 40 ya hisa ya soko kwa muda endelevu, ni ukiukaji wa sheria na hatari ya kuwadhuru washindani na watumiaji.
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za FCC katika kuhakikisha wajasiriamali wanawake wa Kitanzania wanapata maarifa na kujengewa uelewa ili kufanikiwa katika soko la ushindani, ndani na nje ya nchi.
News
Dkt. Biteko akutana na Mtendaji Mkuu wa PUMA Duniani

Na Mwandishi wetu, NewsInfo Online
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Duniani Bw. Mark Russell.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Mei 27, 2025 jijini Dodoma, Dkt. Biteko ameipongeza Kampuni ya PUMA Energies kwa kuwekeza nchini na kutoa huduma ya viwango vya juu katika bidhaa zake pamoja na kuzingatia wazawa katika nafasi za juu za utendaji za Kampuni hiyo nchini.
Vilevile, ametoa rai kwa PUMA Energies kuendelea kuwekeza zaidi nchini na kusema kuwa Kampuni hiyo inaweza kujenga vituo zaidi vya kuweka gesi kwenye magari ili kusaidia upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Kuhusu nishati safi ya kupikia, Dkt. Biteko ametoa wito kwa Kampuni ya PUMA kuwekeza katika eneo hilo na kusema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano wake kwa Kampuni hiyo.
Naye, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Nishati ya PUMA Energies, Bw. Mark Russell amesema kuwa Kampuni yake imewekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 24 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vitatu vya kujaza gesi kwenye magari katika mikoa ya Dar es salaam na kimoja Dodoma.


News
NMB Yatua Mafinga na Kasulu kwa Kijiji Day, Yaendelea Kusambaza Elimu ya Fedha

Na Mwandishi Wetu, NewsInfo Online
Benki ya NMB imeendelea na programu yake ya NMB Kijiji Day kwa kishindo, ambapo matukio mawili makubwa yamefanyika kwa siku moja katika vijiji vya Igowole, Mafinga mkoani Iringa na Rusesa, Kasulu mkoani Kigoma, yakiambatana na utoaji wa elimu ya fedha, huduma za kifedha, elimu ya nishati safi ya kupikia, na kampeni za mazingira.
Katika kijiji cha Igowole, Mafinga, wakazi walipata fursa ya kushiriki katika warsha za elimu ya fedha kupitia mkakati maalum wa Nondo za Pesa, unaolenga kuwafikia Watanzania wengi zaidi katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma rasmi za kifedha. Elimu hiyo ilijumuisha huduma za kufungua akaunti, mikopo, bima na matumizi ya huduma za kidijitali.
Mbali na elimu ya kifedha, tukio hilo lilihusisha semina juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia, mafunzo kwa vyama vya kijamii, burudani kupitia bonanza lenye michezo mbalimbali, na upandaji wa miti zaidi ya 600 kwa ajili ya kuhifadhi mazingira.
Benki iliwakilishwa na Manyilizu Masanja, Meneja wa Mauzo wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, kwa niaba ya Meneja wa Kanda.
Wakati huo huo, katika kijiji cha Rusesa, Kasulu, NMB Kijiji Day ilipamba moto kwa kuwahusisha zaidi ya vikundi 20 vya kijamii vyenye wanachama zaidi ya 600, waliopatiwa elimu juu ya huduma jumuishi za kifedha, nishati safi na utunzaji wa mazingira.
Katika tukio hilo, NMB ilikabidhi na kupanda miche 1,000 ya miti kwenye shule za msingi na sekondari za kijiji hicho, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake kwa Serikali ya Awamu ya Sita kupitia kampeni ya Milioni Moja Miti na mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Katibu Tarafa wa Buyonga Paul Ramadhan alisifu juhudi za NMB katika kuunga mkono mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kuhimiza matumizi ya nishati safi.
“NMB wametushika mkono leo. Tumeshuhudia elimu, michezo, na kampeni za mazingira, all in one. Huu ni mfano bora wa taasisi binafsi kushiriki maendeleo ya jamii,” alisema Ramadhan.
Kwa upande wake, Meneja wa Tawi la NMB Kasulu, Ipyana Mwakatobe, alieleza kufurahishwa na mwamko wa wananchi na kuahidi kuendelea kushirikiana nao ili kukuza ustawi wa kiuchumi, kiafya na kielimu katika wilaya hiyo.
Katika bonanza lililoambatana na sherehe hizo, wakazi wa Rusesa walishiriki michezo mbalimbali ikiwemo kuvuta kamba, mpira wa miguu, mbio za baiskeli, na michezo ya jadi kama bao na drafti. Mechi ya fainali ya mpira wa miguu iliwashuhudia wenyeji Rusesa City FC wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya New Generation Academy ya Kasulu.
NMB inatarajia kufikia zaidi ya vijiji 2,000 kupitia Kijiji Day mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wake wa kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia Watanzania wote, hata walioko vijijini.






-
News10 months ago
Major Sporting Events and International Competitions
-
Science12 months ago
Space Exploration: Recent Discoveries and Future Missions
-
Uncategorized4 weeks ago
NMB Foundation yawanoa Wakulima wa Zao la Kakao Kyela, Serikali yaipongeza
-
Politics11 months ago
Elections 2024: Key Issues and Candidates to Watch
-
Uncategorized1 month ago
NMB Yaandika Historia kwa Kushinda Tuzo Sita Kubwa, Ikiwemo ya “Benki Bora kwa Uendelevu Barani Afrika”
-
Health10 months ago
Mental Health Awareness: Why It Matters More Than Ever
-
News3 weeks ago
Dkt. Biteko akutana na Mtendaji Mkuu wa PUMA Duniani
-
Science11 months ago
Interview with a Scientist: Exploring Cutting-Edge Research