Connect with us

News

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Published

on

Na Mwandishi Wetu, Lindi

VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka vijana nchini kuendelea kulinda amani ya Taifa, kuacha kutegemea taarifa za mitandaoni na badala yake kujitokeza kwa wingi kupiga kura kumchagua kiongozi wanayemtaka katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Wito huo umetolewa leo Oktoba 24, 2025, katika Kongamano la Amani lililofanyika mkoani Lindi, likijumuisha viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.

Katika kongamano hilo, viongozi hao walijadili mada mbalimbali kuhusu umuhimu wa kupiga kura, historia ya chaguzi nchini na wajibu wa kila raia kulingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza katika kongamano hilo, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Sheikh Jamaldin Chamwi, amewataka wananchi kutumia haki yao ya kupiga kura kwa amani na utulivu, akisisitiza kuwa Tanzania ni nchi ya umoja na upendo.

“Kwa yale tunayoyaona mitandaoni, tuwaambie wanaotaka vurugu kwamba Tanzania siyo kama wanavyofikiria. Njia bora ya kuonesha msimamo wetu ni kujitokeza kwa wingi kupiga kura,” amesema Sheikh Chamwi.

Naye Mwakilishi wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Padri Bonavomtura Makota, amesema wanaamini katika nguvu ya vijana na kuwaasa kupokea kile wanachoshauriwa na wazee ili kudumisha amani.

Kwa upande wake kiongozi mwandamizi wa Kamati ya Amani Mkoa wa Ruvuma, Elimu Mwenzegule amesema kuwa wanaunga mkono jitihada za kuhakikisha amani inakuwepo nchini.

Mwenyekiti wa Makanisa Wilaya ya Nachingwea, Mchungaji Leonard John amesema katika historia ya nchi kwa chaguzi zote zilizopita haijawahi kutokea uvunjaji wa amani hivyo kuwaasa viongozi wenzake wa dini kuendelea kufanya jukumu lao la kuhubiri amani.

Abdallah Mpenda ambaye ni Mwenyekiti wa vijana Baraza Kuu ya Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mkoa wa Ruvuma, amesema vijana wanatakiwa kutafakari mambo kabla kuchukua uamuzi ili kuepuka kujazwa chuki na hasira.

“Tusiwe wenye kufanya maamuzi kwa masikio bali kwa tufanye kwa kuona kwa macho yetu, tuangalie hali tuliyokuwa nayo kwenye nchi yetu tunaiona namna gani na kuangalia wale ambao sehemu zao wamekosa amani, wamekosa utulivu, wamekuwa na vurugu, wapo katika hali gani. Halafu tuangalie je tunaweza kumudu yale wanayopitia wenzetu?,” ameeleza Mpenda.

Akichagia mada Mchungaji Lussie Ngongi, amesema ni muhimu viongozi wa dini kuhubiri amani, haki, uhuru kwa watu na kusisitiza kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025.

“Hatuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania, tukumbuke kuilinda Amani ya Taifa letu,” amesema.

Katibu wa Jumuiya ya Vijana Mkoa wa Mtwara, Mussa Khamis amesisitiza kuwa amani ni jambo la msingi kwa ustawi wa kuendesha maisha ya kila siku na kiibada.

“Ili tupate amani lazima tujitokeze siku ya tarehe 29 kupiga kura, kuchagua viongozi ambao tutasaidiana nao katika nchi hii kulinda amani na kuziba upenyo wowote unaoashiria kuvunja amani ya nchi hii,” amesistiza.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.