News

Zahoro Hanuna Achukua Fomu ya Kugombea Ubunge Bumbuli Kupitia CCM

Published

on

Na Mwandishi wetu, News Info Online

Zahoro Rashid Hanuna, leo Juni 28, 2025, amechukua rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hanuna alipowasili katika Ofisi za CCM Wilaya ya Lushoto, mkoani Tanga, alipokelewa na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mhe. M.S. Kaaya, ambaye alimkabidhi rasmi fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Hanuna si mgeni katika siasa za ndani ya CCM. Mwaka 2020 aligombea kura za maoni katika Jimbo la Kawe, na mwaka 2021 alijitokeza kuwania nafasi ya uspika wa Bunge kupitia chama hicho.

Hatua yake ya kuchukua fomu leo inaashiria mwendelezo wa safari yake ya kisiasa, akilenga kuwawakilisha wananchi wa Bumbuli bungeni kupitia tiketi ya CCM

0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

Trending

Exit mobile version