Connect with us

News

NMB yatoa 500m/- kusaidia matibabu ya moyo ya watoto 125 nchini

Published

on

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online

Benki ya NMB tayari imetoa nusu ya TZS bilioni 1 ilizoahidi mwaka jana kwa ajili ya kuiwezesha Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kutoa matibabu ya moyo ya watoto 250 katika kipindi cha miaka minne, hatua ambayo imesaidia kubadili maisha ya familia zisizojiweza nchini.

Ahadi hiyo, iliyotolewa tarehe 2 Novemba mwaka jana, inalenga kugharamia upasuaji na matibabu ya watoto wanaokabiliwa na magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo na matatizo mengine ya mfumo wa moyo, hususan wale wanaotoka katika familia zenye kipato duni.

Jana, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna, aliongoza ujumbe wa maafisa waandamizi wa benki hiyo kutembelea JKCI, ambapo alitangaza kuwa benki hiyo imeshatoa TZS milioni 500 ambayo ni sawa na nusu ya ahadi yote.

Kwa mujibu wa Bi Zaipuna, kiasi hicho kimesaidia kuwezesha upasuaji na matibabu ya moyo ya watoto 125.

“Tunawashukuru sana JKCI kwa kazi yao ya kipekee ya kufanya upasuaji huuna tunaahidi kuendeleza ushirikiano huu ili kuwasaidia Watanzania hasa familia zisizojiweza kupata matibabu na huduma stahiki,” alsiema.

Aliongeza kuwa kiasi kingine cha TZS milioni 250 kitatolewa Januari mwakani ili kuhakikisha mchakato wa matibabu magonjwa ya moyo ya ya watoto unaoendelea na kufanyika bila kukwama.

Bi Zaipuna pia alisisitiza kuwa msaada wa NMB hauishii kwenye fedha pekee.

Benki hiyo itaendelea kuimarisha ushirikiano wake na JKCI, Heart Team Africa Foundation, na Global Medicare ili kupanua wigo wa huduma, kuongeza kasi ya upasuaji, na kuimarisha miundombinu ya huduma za moyo kwa watoto.

Moja ya mapendekezo na maombi aliyoyapokea ni suala la kuanzisha “Recovery House” — kituo maalum cha kuwapokea watoto wanaosubiri upasuaji au kuendelea na matibabu — ambacho kitasaidia kupunguza mzigo wa kifedha na changamoto za makaazi kwa familia kutoka maeneo ya mbali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dkt. Peter Kisenge, alisema NMB imekuwa mdau namba moja katika kusaidia familia zisizojiweza kupata huduma muhimu za moyo.

Bingwa huyo wa magonjwa ya moyo alibainisha kuwa mchango wa benki hiyoumeongeza ufanisi wa huduma, kupunguza muda wa kusubiri na kuongeza idadi ya watoto wanaoweza kutibiwa kila mwaka.

Kwa upande wake, Afisa Mgtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation, Dkt. Naizihijwa Majani, alisema ufadhili wa NMB umewanufaisha watoto kutoka mikoa 20.

“Kati ya upasuaji 185 uliofanyika mwaka huu, 125 wamefadhiliwa na NMB — jambo linalothibitisha ukubwa wa uhitaji na thamani ya msaada unaotolewa kwa wakati,” alibainisha.

Kwa akina mama Veronica Temba na Asimina Issa kutoka Kilimanjaro, msaada huo umekuwa mwanga wa matumaini. Wakiwa hawana uwezo wa kugharamia upasuaji wa moyo, waliuelezea mchango wa NMB kama “baraka ya kweli” kwa familia zao.

Wameiomba benki hiyo kuendeleza moyo huo wa ukarimu ili familia nyingine nyingi zisizo na uwezo ziendelee kunufaika na ufadhili wa matibabu ya moyo – ufadhili ambao kwa wengi wao ndio tofauti kati ya kukata tamaa na kupata matumaini mapya ya maisha.

Ziara hiyo ilibainisha ukweli muhimu: mpango wa NMB wa kusaidia matibabu ya moyo ya watoto sio tu jukumu la kijamii — ni uwekezaji katika kizazi kijacho cha Tanzania, na katika maisha ya watoto ambao vinginevyo wangeachwa bila matumaini.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.