Connect with us

News

Rais Samia Aleta Mapinduzi ya Ustahimilivu wa Tabianchi: Tanzania Yapata Dola Milioni 9.38 Kulinda Wakulima wa Mkondoa dhidi ya Mafuriko na Ukame

Published

on

Na Mwandishi wetu, News Info Online

SERIKALI ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha mafanikio makubwa katika diplomasia ya maendeleo na usimamizi wa uchumi kwa vitendo.

Hivi karibuni, Mfuko wa Maendeleo wa Afrika (African Development Fund) umeidhinisha ufadhili wa takribani dola za Marekani milioni 9.38 kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa Tanzania kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi katika Bonde la Mto Mkondoa.

Ufadhili huu umetolewa kupitia dirisha maalum la Climate Action Window, hatua inayohakisi imani na heshima kubwa ambayo taasisi za kimataifa zinaendelea kuiweka Tanzania kutokana na sera madhubuti, diplomasia shirikishi na uongozi thabiti wa Rais Dkt.Samia.

Mradi huu unalenga kulinda maisha ya wananchi, kuimarisha shughuli za kilimo na kuhifadhi miundombinu muhimu dhidi ya athari za mafuriko na ukame unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Mradi huu una lengo la kulinda jamii zilizo hatarini na miundombinu muhimu kutokana na mafuriko na ukame unaosababishwa na hali ya hewa inayobadilika.

Aidha,manufaa makuu ya mradi ni kulinda maisha na biashara za wakulima dhidi ya mafuriko na ukame.

Pia,kuimarisha mifumo ya tahadhari mapema na ujenzi wa miundombinu imara dhidi ya hali ya mabadiliko ya tabianchi kama vizingiti na mabwawa madogo.

Faida nyingine ni urekebishaji na kurejesha ardhi hekta 1,200 zilizoharibika ikiwemo kufungua fursa za ajira takriban 3,500 kazi za muda na 1,000 ajira za kudumu, hasa kwa wanawake na vijana. ⁠

Vilevile,mradi utaleta faida kwa wanaume, wanawake na familia 774,000 wanaoishi katika wilaya za Gairo, Kilosa na Mvomero mkoani Morogoro.

Mradi huu utatekelezwa na Wami/Ruvu Basin Water Board chini ya Wizara ya Maji, na kazi itaanza Januari,2026.

U⁠natarajiwa kuboresha usalama wa maji kwa matumizi ya kaya na kilimo, kupunguza umaskini, kuimarisha usalama wa chakula na kusaidia ukuaji wa uchumi endelevu pamoja na kulinda barabara ya kimkakati ya Morogoro–Dodoma (B-127).

Kupatikana kwa ufadhili huu ni ushahidi wa mafanikio ya diplomasia ya kiuchumi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita, ambapo Tanzania imefanikiwa kujenga ushirikiano imara na wadau wa maendeleo, kuvutia rasilimali za kimataifa, na kuelekeza misaada hiyo kwenye miradi yenye tija kwa maendeleo ya wananchi.

Pia, mradi wa mto Mkondoa unaonesha kwa vitendo dhamira ya Rais Dkt.Samia ya kuhakikisha maendeleo endelevu, ulinzi wa mazingira, na ustawi wa wananchi vinaenda sambamba.

Hiki ni kielelezo tosha kwamba uongozi makini, diplomasia yenye tija na sera bora za kiuchumi vinaweza kuleta matokeo chanya yanayogusa maisha ya watu moja kwa moja.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.