Connect with us

News

Sekta ya Afya Yapiga Hatua Kubwa, Serikali Yatakiwa Kuongeza Nguvu Vijijini

Published

on

Na Mwandishi wetu, News Info Online

Mkurugenzi Mkuu wa Health Africa Events, Dkt. Mshana Abdallah, amesema sekta ya afya nchini Tanzania imeendelea kuimarika kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na miaka ya nyuma, huku akieleza kuwa ongezeko la vituo vya afya, hospitali kubwa pamoja na kuanzishwa kwa teknolojia mpya za kitabibu ni miongoni mwa viashiria vya maendeleo hayo.

Akizungumza wakati wa utoaji wa Tuzo za Health Africa Awards, Dkt. Mshana alisema tuzo hizo ni jukwaa maalumu lililoandaliwa kwa lengo la kutambua na kuthamini juhudi, ubora na jitihada zinazofanywa na taasisi mbalimbali za afya, mashirika, wawekezaji pamoja na wadau wote wa sekta ya afya nchini.

Aliongeza kuwa kwa sasa sekta ya afya imekua kwa upana zaidi, huku maeneo yanayohitaji maboresho yakiwa ni machache sana. Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa serikali kuendelea kuweka mkazo katika kuboresha huduma za afya vijijini, hususan kuhakikisha upatikanaji wa madaktari na wataalamu wa afya katika vituo vilivyopo maeneo ya pembezoni.

Dkt. Mshana alisema utoaji wa tuzo hizo ni mara ya kwanza kufanyika, lakini utakuwa ni mwanzo wa safari endelevu ya kuhamasisha ubora katika sekta ya afya. “Niwapongeze washiriki wote waliopata tuzo leo, na tunatarajia kuona huduma bora zaidi za afya zikiendelea kutolewa nchini,” alisema.

Kwa upande wake, Dkt. Patric Shao, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura na Ajali kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili na pia Mweka Hazina wa Chama cha Madaktari wa Dharura Tanzania (IMAT), alisema huduma za dharura ni muhimu kwa kiwango kikubwa kwa sababu dharura haziwezi kupangwa.

Alisisitiza umuhimu wa jamii kuwa na uelewa wa mbinu za awali za kuwahudumia wagonjwa wanaopata dharura za kiafya au ajali ili kusaidia kuokoa maisha.

Aliongeza kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili imekuwa ikiendesha mafunzo mbalimbali kwa watoa huduma za afya pamoja na makundi ya kijamii ili kuwajengea uwezo wa namna ya kuchukua hatua za haraka na sahihi wakati wa dharura za kiafya.

Naye Dkt. Nicas Mawazo, bingwa wa juu (super specialist) wa huduma za uzazi kwa njia ya IVF, alisema tuzo waliyoipata si ya bahati mbaya bali ni matokeo ya kazi kubwa wanayoifanya. “Watanzania wametuamini na wamethibitisha kuwa tunatoa huduma bora. Tutaendelea kutoa huduma zenye viwango vya juu zaidi kila siku,” alisema.

Dkt. Mawazo aliongeza kuwa taasisi yao ni jawabu kwa familia nyingi zilizokosa watoto, akisisitiza kuwa katika dunia ya sasa hakuna lisilowezekana. “Hakuna mwanaume asiyestahili kuitwa baba wala mwanamke kuitwa mama. Mafanikio yetu ni mengi, watu wengi wamepata faraja na watoto kupitia kliniki zetu,” alisema.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Idara ya Biashara, Masoko na Mawasiliano kutoka Taasisi ya Afya ya Aga Khan Tanzania Olayce Loatha alisema wamepokea kwa furaha kubwa tuzo ya mwaka 2025, akieleza kuwa ni ushuhuda kuwa Tanzania ina hospitali nyingi za umma na binafsi zinazotoa huduma bora za afya kwa viwango vya juu vya usalama na uangalizi.

Alisema tuzo hiyo ni motisha ya kuongeza juhudi, uwajibikaji na nguvu katika kuwahudumia Watanzania, akisisitiza lengo lao ni kuhakikisha hakuna mgonjwa anayeingia hospitalini hapo na kupoteza maisha. Pia alibainisha kuwa taasisi hiyo inaunga mkono jitihada za serikali katika kukuza utalii wa tiba (medical tourism), kwa kutoa huduma sawa na bora kwa Watanzania na wageni wanaofika nchini.

“Tunajivunia kuwa miongoni mwa hospitali zinazochangia kulifanya Taifa letu livutie katika huduma za kitabibu, na tutaendelea kuboresha huduma zetu kila wakati,” alisema.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.