Connect with us

News

TotalEnergies wazindua kituo kipya cha mafuta Kimara

Published

on

Kampuni ya TotalEnergies Marketing Tanzania imezindua rasmi kituo chake kipya cha kisasa cha mafuta, TotalEnergies Kimara Service Station, kilichopo Kimara, jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo umeashiria mwanzo wa huduma bora zaidi kwa wateja wa eneo hilo na maeneo ya jirani, kwa kuwapatia mafuta ya ubora wa juu na huduma za uhakika.

Kituo hicho kipya kinalenga kubadilisha kabisa uzoefu wa utoaji huduma za mafuta kwa wakazi wa Kimara na wasafiri, kikitoa bidhaa na huduma mbalimbali ikiwemo mafuta ya Excellium, huduma ya Fuel Card, mafuta laini ya ubora wa juu (lubricants) pamoja na gesi ya kupikia ya TotalEnergies.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo huku katika wiki ya huduma kwa wateja Afrika iliyoenda sambamba na kaulimbiu isemayo ‘Imani yako kwetu, nguvu yetu kila siku’ Mkurugenzi Mtendaji wa TotalEnergies Marketing Tanzania, Bw. Mamadou Ngom, alisema kuwa uzinduzi wa kituo hicho unaenda sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja Afrika 2025, ambayo inalenga kuthamini na kuimarisha uhusiano wa kampuni hiyo na wateja wake.

“Tunapozindua rasmi Kituo cha Huduma cha Kimara, tunasherehekea pia kuanza kwa Wiki ya Huduma kwa Wateja Afrika. Kaulimbiu ya mwaka huu ‘Your Trust, Our Everyday Energy’ inatukumbusha kuwa mafanikio yetu yanatokana na imani ya wateja wetu kwetu,” alisema Bw. Ngom.

Aidha, Bw. Ngom aliongeza kuwa ufunguzi wa kituo hicho ni uthibitisho wa dhamira ya TotalEnergies ya kusogeza huduma za nishati karibu zaidi na wananchi kupitia mpango wake wa Dealer-Owned-Dealer-Operated (DODO), ambao unalenga kupanua mtandao wa vituo vya mafuta nchini kote.

“Kituo cha Kimara ni alama ya uaminifu, ushirikiano na maendeleo misingi ambayo inatuongoza kila siku,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Bw. Godfrey Nyashage, ambaye ni mmiliki na msimamizi wa kituo hicho, alieleza furaha yake kuona ndoto yake ikitimia kwa kushirikiana na kampuni ya TotalEnergies.

“Niliamua kushirikiana na TotalEnergies kwa sababu naamini katika nguvu ya chapa yao na maadili wanayosimamia. Ushirikiano huu sio tu biashara, bali ni uhusiano wa kuaminiana na kujituma kutoa huduma bora kwa wateja wetu,” alisema Bw. Nyashage.

Aidha alisema ndani ya miaka mitatu ijayo anategemea kuwa na vituo zaidi ya vitatu ili aendelee kuwekeza ndani na hivyo kuweza kukuza uchumi wa Tanzania.

Kadhalika alisema mazingira ya uwekezaji kwa Tanzania ni mazuri kutokana na standard zake huku akiiomba serikali kuendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji yasiyo na usumbufu

Naye Juma Mohammed katibu wa umoja wa madereva bajaji-kwa Msuguli alishukuru ujio wa mradi huo kwani umewarahisishia upatikanaji wa mafuta kwa ukaribu hivyo wameondokana na adha ya kuzunguka kwa umbali mrefu kupata huduma hiyo

Uzinduzi wa TotalEnergies Kimara Service Station ni hatua muhimu katika safari ya kampuni hiyo ya kusogeza huduma za nishati bora karibu na wananchi, huku ikiendelea kupanua uwepo wake kote nchini Tanzania kupitia ushirikiano imara na mtazamo wa kumjali mteja.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.