Connect with us

News

Viongozi wa dini Kaskazini wahimiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Published

on

Na Mwandishi wetu, Newsinfo Online

VIONGOZI wa dini kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini, wamewataka Watanzania kulinda amani ya nchi, hasa taifa linapoelekea katika Uchaguzi Mkuu, wakisisitiza kuwa amani ni nguzo muhimu kwa ustawi wa taifa.

Viongozi hao kutoka mikoa ya Tanga, Arusha, Manyara na Kilimanjaro wametoa kauli hiyo leo Oktoba 22, 2025 katika Kongamano la Amani na Uchaguzi lililofanyika mjini Moshi.

Mwishoni mwa kongamano hilo lililoongozwa na kauli mbiu ‘Kupiga kura ni haki yetu na amani ya nchi yetu ni wajibu wetu’, viongozi wa Dini wamesoma maazimio, yanayosisitiza ulinzi wa amani ya nchi na kuhimiza wananchi kushiriki katika uchahuzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akisoma maazimio hayo, Katibu wa BAKWATA Wilaya ya Moshi, Alhaji Awadhi Lema ametaja mambo saba yaliyokubaliwa na viongozi wa dini kuwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi waliojiandikisha kuhakiki majina yao na kujitokeza kupiga kura.

Azimio jingine ni kuwataka Watanzania kuepuka uchochezi kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari, Vyombo vya dola kutumia hekima na busara kulinda amani siku ya uchaguzi, kupanua ushiriki wa viongozi wa dini katika vyombo vya maamuzi na utungaji wa sheria pamoja na kila mwananchi kuwa na wajibu wa kulinda amani wakati wa kudai haki yake.

Akizungumza katika Kongamano hilo, Sheikh wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mlewa Shaban, amesema hakuna amani ya kweli bila haki, usalama wa uhai na mali.

Amefafanua kuwa, jukumu la kulinda amani si la serikali pekee bali ni la kila raia, akisisitiza umuhimu wa kuepuka chuki, uongo na maneno ya kuchochea mgawanyiko.

“Kuua mtu mmoja ni sawa na kuondoa amani kwa jamii nzima na raia mwema ni yule anayejenga amani kwa wengine. Amani hujengwa kwa uvumilivu, uadilifu na kuheshimiana bila kujali tofauti za kidini, kikabila au kisiasa,” amesema Sheikh Mlewa.

Mwanasheria wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Mch. Wakili Daniel Swai aliyemwakilisha Askofu Fredrick Shoo, amesema amani na haki haviwezi kutenganishwa, kwani vinashikamana katika kujenga jamii yenye heshima na mshikamano.

Naye Padri Steven Msami kutoka Kanisa la Anglikana Tanga amesema amani ni tunda takatifu, na palipo na amani watu hukaa kwa utulivu.

“Tusiseme amani tu, bali tuseme na uvumilivu, kwani bila uvumilivu hakuna amani,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Elinawinga Mariki amewataka wananchi kujitokeza kujiandikisha na kushiriki uchaguzi ili kupata viongozi wenye hekima na busara.

Katibu wa Bakwata, Mkoa wa Arusha, Ally Athuman Nassoro, amesisitiza kuwa amani haina mbadala, hivyo Watanzania wanapaswa kuilinda kila wakati wanapokutana na changamoto.

“Tumuombe Mungu atupe uongozi utakaoleta maisha bora kwa Watanzania,” amesema.

Yakoba Hassan, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kinamama Waislamu Moshi, aliomba vyombo vya ulinzi na usalama kuepuka kutumia nguvu kupita kiasi wakati wa uchaguzi, ili kudumisha amani iliyopo.

Awali akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mzava, amesema Tanzania inaelekea kwenye uchaguzi wa kikatiba na kidemokrasia huku hali ya amani ikiendelea kutawala mkoani humo.

“Tunaendelea kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura kwa sababu ni haki yao ya msingi. Serikali itahakikisha usalama na haki vinatawala katika mchakato mzima wa uchaguzi,” alisema Mzava.

Aliongeza kuwa serikali inafarijika kuona viongozi wa dini wanashirikiana katika kulinda amani, kwani maoni na ushauri wao ni mchango muhimu kwa serikali na jamii.

Continue Reading
Click to comment
0 0 votes
Article Rating
Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments

News

Wanawake 142 waanza mafunzo ya Female Future Programme Dar es Salaam

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wanawake 142 wamepokelewa rasmi kushiriki toleo la 12 la programu ya mafunzo ya uongozi kwa wanawake, Female Future Programme (FFP), iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo ya kiutendaji yameandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kwa kushirikiana na Taasisi ya Usimamizi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI).

Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran amesema programu hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa zaidi ya wanawake 800 waliokwisha pata mafunzo kwa zaidi ya muongo mmoja, na sasa inaendeshwa katika nchi sita kwa ufadhili wa NHO, huku akiwahamasisha washiriki kushiriki kikamilifu safari ya miezi tisa ya mafunzo. Aidha, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ESAMI, Dkt. David Kalaba amesema jamii inahitaji wanawake viongozi wenye kujiamini na uwezo mkubwa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya haraka, akisisitiza umuhimu wa mtazamo wa kimataifa, kujifunza na kuendana na mabadiliko pamoja na uwezo wa kusimamia utofauti, kutatua migogoro na kutoa thamani kwa wateja.

Kwa upande wake, Meneja wa Upstream wa IFC, Bw. Sam Nganga aliyemwakilisha Meneja wa Nchi, Bi. Martine Valcin amesema taasisi hiyo inaendelea kuhakikisha wanawake wanapewa nafasi katika ngazi za juu za uongozi ili kukuza ushirikishwaji, huku akiwahimiza washiriki kujisimamia na kutumia kikamilifu mafunzo hayo.

Katika hafla hiyo pia kulikuwa na mjadala wa jopo kuhusu wanawake katika uongozi uliowashirikisha wataalamu mbalimbali wa rasilimali watu na uongozi kutoka taasisi tofauti, ambapo ilisisitizwa kuwa kuchanganya uzoefu wa vizazi tofauti vya wanawake kazini huleta matokeo chanya pamoja na umuhimu wa kujifunza ujuzi mpya na kuimarisha mentorship baada ya mafunzo.

Washiriki wa kundi la 12 walihimizwa kujenga mitandao imara ya kitaaluma, huku taasisi na makampuni yakitakiwa kutambua upekee wa kila mwanamke badala ya kuwaona kama kundi moja.

Akihitimisha, Mjumbe wa Bodi ya ATE, Bw. Gasper Kikui amesema sekta isiyo rasmi bado ina changamoto nyingi za uongozi na kuwataka washiriki kuyachukulia mafunzo hayo kwa uzito ili kuleta mabadiliko chanya.

Continue Reading

News

Dkt Samia: Vijana wanufaike na uwekezaji katika mawasiliano

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka vijana wanufaike ipasavyo na huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano, hasa katika maeneo ya kukuza ubunifu, ujuzi wa kidigitali na fursa za ajira.

Ametaka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, zishirikiane na wadau wa sekta ya teknolojia ili vijana wapate manufaa hayo.

Dkt Samia ameyasema hayo leo, Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi huo, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85.

“Uwekezaji huu kwa vijana ni muhimu kwa sababu dunia ya teknolojia ni ya kwao. Dunia hii ipo viganjani mwao na ndiyo mfumo wa maisha yao. Ni lazima tuwawezeshe na kuwahamasisha kutumia mifumo hii ili waweze kukua kiuchumi na kijamii,” amesema.

Continue Reading

News

Dkt Samia azindua minara 758, kuwanufaisha zaidi ya wananchi milioni nane

Published

on

By

Na Mwandishi wetu, News info

Zaidi ya wananchi milioni 8.5 hususan wanaoishi mipakani na vijijini, wanatarajiwa kuondolewa changamoto ya mtandao, baada ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kuzindua minara 758 ya mawasiliano iliyojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Uzinduzi huo umefanyika leo Ijumaa Aprili 10, 2026 jijini Dodoma, ukiambatana na kuunganisha huduma za mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 85, ikiwa ni juhudi za Serikali kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza huduma za mawasiliano.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt Samia amesema uwekezaji huo umetokana na ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta ya mawasiliano ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi kwa ubora unaokidhi mahitaji ya teknolojia ya kisasa na kwa gharama nafuu.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa minara hiyo kutachochea ushiriki wa wananchi katika uchumi wa kidijitali na kufungua fursa mpya za ajira, kuboresha utoaji wa huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Mawasiliano si tena huduma ya anasa kama ilivyokuwa zamani. Leo hii ni uti wa mgongo wa uchumi wa kisasa na daraja la fursa kwa wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo,” amesema

Continue Reading

Trending

Copyright © 2025 Newsinfo.